Jumanne, 14 Mei 2013

MAOMBI YA NAFASI YA KAMISHINA MKUU

Chama cha SKAUTI Tanzania kinakaribisha maombi ya kugombea nafasi ya KAMISHINA MKUU.
Katika kikao chake cha Viongozi waandamizi (Skauti Mkuu, Kamati Tendaji, Kamati ya Mpito na Wakufunzi) kilichofanyika tarehe 09 Mei, 2013 chini ya Uenyekiti wa Skauti Mkuu Mh. Mwantum Mahiza kimeazimia mambo yamsingi yafuatayo:-

  • ·     Kutangaza kimaandishi nafasi iliyowazi ya Kamishna Mkuu.  Hii ni nyongeza ya tangazo alilolitoa Skauti Mkuu katika Mkutano wake na viongozi mbali mbali jijini Dar es Salaam uliofanyika tarehe 06 Mei 2013.
  • ·    Kutoa sifa na fomu za kugombea.

Sifa na Fomu za kugombea nafasi hiyo zinatolewa Makao Makuu ya Chama kuanzia tarehe 10 Mei, 2013.   
Pia zinapatikana katika www.DaresSalaamlocalscout.blogspot.com Search Google: - Dar Es Salaam Local Scouts Association.  Fomu zinaweza kurejeshwa kwa njia zifuatazo:-

-      Kwa “Despatch” kwa Mwenyekiti au Karani wake, Makao Makuu ya Chama.
-      Kwa “Registered Mail – Mwenyekiti wa Kamati ya mpito, Chama cha Skauti Tanzania S.L.P 945 DSM.
-      Kwa E-mail:szone2012@live.com

Mwisho wa kurejesha fomu ni tarehe 20 Mei 2013, saa 10.00 jioni.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Mpito Brigedia Jenerali Mstaafu Gerald Mkude, ameelezea sifa za mwombaji wa nafasi hiyo ni:-
 
1.           Awe Kamishna au aliwahi kuwa Kamishna

2.           Awe Mtanzania

3.           Awe hajawahi kuachishwa uongozi katika Chama cha Skauti au kushitakiwa kwa makosa ya jinai kwa kipindi cha miaka minne (4) iliyopita.

4.           Awe ametunukiwa Nishani ya Skauta (Woodbadge Holder)

5.           Awe na Elimu ya Sekondari au zaidi.

6.           Awe na uzoefu wa uongozi na utawala katika shughuli za Skauti na jamii kwa ujumla kwa muda usiopungua miaka 5.

7.           Awe ametoa mchango mkubwa wa huduma kwa Chama cha Skauti na jamii kwa ujumla.

8.           Awe ana uwezo wa kusimamia, kulinda na kutetea Katiba na Kanuni za Skauti wakati wote.

9.           Awe mtu wa kujiamini na kujitambua.

10.       Awe mweledi na mwaminifu

11.       Awe na uwezo wa mawasiliano Kitaifa na kimataifa.

12.       Awe mwenye umri wa miaka 35 au zaidi

Mwombaji atajaza Fomu iliyotayarishwa, pia alete maelezo yake binafsi yaani C.V. yake.

Pamoja na hayo, fomu ya kugombea nafasi hiyo inapatikana kwa kiitroniki katika ukurasa wa Facebook wa Dar Es Salaam Scout, bonfya hapa: http://www.facebook.com/#!/groups/171718552973513/

Fomu hiyo ipo katik utaratibu ufuatao:-
 
FOMU YA KUGOMBEA NAFASI YA KAMISHNA MKUU

FOMU NO: …………..

SEHEMU (A): MAELEZO BINAFSI (HERUFI KUBWA)

1.  JINA KAMILI   ……………………………………………………………….
2.  UMRI   …………………...  MAKAZI ……………………………         
3.  ELIMU ………………………………………………………………………….
4.  KAZI    …………………………………  MAHALI  ………………………
5.  ANUANI YA POSTA    ……………………………………………………
6.  SIMU   ……………………  EMAIL  ………………………………………
  1. UZOEFU WA UONGOZI
……………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………

  1. SAHIHI ………………………………………………….
SEHEMU (B):      MAONI YA KIKAO CHA UCHAMBUZI
……………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………

SAHIHI YA MWENYEKITI/KATIBU……………………………….. TAREHE …………….

SEHEMU (C):      MATOKEO YA UCHAMBUZI
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………

SAHIHI YA MWENYEKITI/KATIBU……………………………….. 
TAREHE ……………………

 
Mwisho wa kurejesha fomu ni tarehe 20 Mei 2013, saa 10.00 jioni.