Alhamisi, 27 Juni 2013

SKAUTI MKUU AAPISHWA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgbHxvklKnvoZvn4A4BM5KGRr6tXB4Lm0eJRw0YtYQabZv0QZbdzI3ROHJXXxTThY1-OTkbkc4bGcOOlRYDi2DB-3cos8lkE-v9B5lohCeiljH21wfRF4vk6e-A4pgRnRM9W4LsNgnEMIc/s1600/sk4.jpg
Rais Dkt.Jakaya Kikwete akimuapisha Skauti Mkuu Mhe. Mwantum Mahiza Ikulu Juni 24, 2013


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemuapishwa Skauti Mkuu wa Tanzania siku ya Juma tatu tarehe 24 Juni, 2013 Ikulu jijini Dar Es Salaam.
Kuapishwa kwa Skauti Mkuu ni tukio kubwa lililokuwa linasubiriwa na skauti Tanzania, kwani chama kimekaa kwa muda mrefu bila kuwa na kiongozi, pamoja na hilo, kuapishwa kwa Mhe. Mwantum Mahiza kuwa Skauti Mkuu ni historia kwa Skauti Tanzania kwani yeye ndiyo mwanamke wa kwanza kushika nafasi hiyo kwa Tanzania.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjjOJD7XT-X36KMrSX0cqcW3T5LOnTMBcQc7FJVemupcBXPd2IiN0qXOZgtiV4cMKHesf_m1eQGhpCEwA6RYZ3iXc0yAGIIKnOWfIqTPVQ1LubmnqfdG9uFwT5X4rcKUVo4yzcR9Mw3rhE/s1600/sk5.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka sahihi baada ya kumuapishwa Skauti Mkuu Mhe. Mwantum Mahiza Ikulu jijini Dar Es Salaam, Juni 24, 2013.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidUi7sitXHwfnh9omohTNBZhUKEiDzY-m9sWjXQ7quErTsf8AIBXw6-EgnTt4jBZFSCDhWSto9n4R4BE-_jkAm4YPKAXxEdyaNdv3DYGIT4aDsySyVkbEVQ0uLKVqBikEyYQfB428rtt4/s1600/sk6.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi vitendea kazi baada ya kumwapisha Skauti Mkuu Mhe. Mwantum Mahiza ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgdAcj8wbKYBW8_usGXE1tKr0RUJemu4w_YY5rBnBJa4rqpnzrkodxTP2QyHfrnpFzLY6LmApOkhGwt-XAAzhBQJNUXWDGzRUjOM43i1sH7N4VMi88EDvgOQUvl7XXaQPPs2zxmT4dqa64/s1600/sk7.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Skauti Mkuu Mhe. Mwantum Mahiza baada ya kumwapishwa Ikulu jijini Dar Es Salaam Juni 24, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 24, 2013

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim, Jaji Kiongozi Fakih Jundu na Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 24, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza pamoja na viongozi wa maskatu na skauti  baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 24, 2013

Katika hafla hiyo ya kumwapishwa Skauti Mkuu pia iliudhuliwa na Skauti Wabunge wa Tanzania wakiongozwa na Mwenyekiti wao Mhe. Abdulkarim Shah (Mbunge wa Mafia)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza pamoja na waheshimiwa wabunge ambao ni maskauti  baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 24, 2013
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na skauti Ismail Aden Rageh na wabunge maskauti  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 24, 2013

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha na  Skauti Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Mwantumu Mahiza na viongozi wa skauti nchini baada ya kumuapisha  Ikulu jijini Dar es salaam Jumatatu Juni 24, 2013
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjJBL8Sevl38-a8RD6ZdDHvcrM0CHO6e9Z2cQFe3stPmaBVxHkRhMZWLuMd-HUZwVCBgJ4KOZ9yIMRCRYtYPbaBbG8yQUFZu51uz4uUEZHQh_N4t4nRqdc6xq7AivyBu-S7UFWLEGQgc7s/s1600/sk3.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akivishwa skafu na Skauti kabla ya kumwapishwa Skauti Mkuu Mhe. Mwantum Mahiza jijini Dar Es Salaam Juni 24, 2013
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi7Gcyvh35XI8qK7ySsn232ovdzq6EprXFM7mK7-AboQqMyX5utjXvj7taDNQpvvcrTGhppd5Noqqyoc0nEyT9TYTlPCpLQAzybjpYD74IfhHZBlSmxhROTAJ8BvuM6ZaM1HAqkn_ERklM/s1600/sk1.jpg
Skauti Mkuu mhe. Mwantum Mahiza akisubiria kuapishwa akiwa na Skauti Wabunge na Viongozi wengine wa Skauti Tanzania, Juni 24, 2013 Ikulu jijini Dar Es Salaam.

Jumanne, 11 Juni 2013

MKUTANO MKUU WA UMOJA WA WABUNGE SKAUTI DUNIANI

Wajumbe kutoka Japan na Korea wakijadiliana maandalizi ya Mkutano wa 7 wa umoja wa skauti wabunge duniani 2011.
  • Maandalizi ya Mkutano wa 7 wa Umoja wa Wabunge Skauti Duniani!

Wawakirishi wa Chama cha Skauti Japan (Scout Association of Japan - SAJ) mwaka 2011 walienda Korea kwa ajili ya maandalizi ya mkutano mkuu wa Umoja wa Skauti Wabunge Duniani "World Scout Parliamentary Union (WSPU)" ambao utafanyika nchini Japan mwaka 2013. Wawakirikishi wa Chama cha Skauti Japan (SAJ) pamoja kukutana na wawakilishi wa Chama cha Skauti Korea (KSA) pia walikutana na wawakilishi wa umoja wa wabunge Skauti wa nchini Korea (Korean Scout Parliamentary Association - KSPA) ambao wanafanyakazi kama Kamati Tendaji ya Umoja wa Wabunge Skauti Duniani.

Mh. Abdulkarim Shah Mwenyekiti wa Wabunge Skauti Tanzania (Mbunge wa Mafia)
Madhumuni makubwa ya ziara ya wawkilishi wa SAJ yalikuwa ni kubadilishana habari na uzoefu wa kiutendaji kuelekea mkutano mkuu wa saba wa umoja wa wabunge skauti unaotarajiwa kuudhuliwa na wabunge skauti kutoka nchi tofauti duniani watakao jadili mada kuhusu Skauti na Vijana, pamoja na vijana kushiriki katika maamuzi yatakayoleta tija miongoni mwao.

Uzoefu umepatikana toka Chama cha Skauti Korea (KSA) na Umoja wa Wabunge Skauti wa Korea (KSPA) katika Mkutano Mkuu wa 6 Duniani uliofanyika nchini Korea, katika ziara hiyo walijadiliana katika nyanja tofauti kama mipango na mikakati. Pamoja na hayo, pia Mkutano Mkuu pia mkutano mkuu wa 6 nchini Korea ulijadili miundo na mipangilio ya kamati za shughuli/matukio, pamoja na bajeti na udhamini.

Kwa ajili ya mpangilio mzuri wa mkutano huu nchini Japan, SAJ imeanza maandalizi mapema toka mwaka 2011, na pia itakuwa mwenyeji wa Jamboree ya Skauti ya 23 ya Dunia (WSJ) ambao utafanyika mwezi Julai mpaka Augosti 2015. Kwa kutambua umuhimu na ukubwa wa tukio, Chama cha Skauti Japan (SAJ) pia kimeanza maandalizi ya 30th Asia-Pacific Regional Scout Jamboree na 16th Nippon (National) Jamboree.

Kikubwa cha kujifunza kutoka kwa wenzetu ni umuhimu wa maandalizi ya mikutano na shughuli mbalimbali, Mkutano mkuu wa 7 wa Umoja wa Wabunge Skauti Duniani, Japan imeanza maandalizi toka mwaka 2011 ambapo utafanyika mwaka 2013 mwezi Novemba.

Huenda hata TSA hawana habari au maandalizi yeyote kwa Wabunge Skauti wa Tanzania kushiriki mkutano huu. Hata hivyo jitihada zinaendelea za kumtafuta muhusika wa TSA na mwenyekiti wa Wabunge Skauti Tanzania Mh. Abdulkarim Shah (Mbunge Wilaya ya Mafia) kutupa ufafanuzi juu ya hili.




Kwa habari zaidi wasiliana na:
The World Scout Parliamentary Union (WSPU)
The Scout Association of Japan (SAJ)
The 23rd World Scout Jamboree 2015

The World Scout Parliamentary Union (WSPU) is an international organisation that unites the National Scout Parliamentary Associations (NSPAs) which exist in almost 100 countries world-wide and their members are Members of national Parliaments, Deputies or Senators. Its object is to strengthen National Scout Organisations and World Scouting through the influence of parliamentarians who believe that Scouting is an effective educational method.
Each NSPA decides independently on the membership and organizational form of a given NSPA. In some countries this structure is formalized; in others it is quite casual; some even include members of Regional Parliaments. In all cases, however, a fundamental principle of balanced political representation must be - and is - ensured: an NSPA's membership scheme should never be in favour of one party.
The catalyst for the creation of WSPU was the opportunity to use the untapped support that existed in parliaments and governments for World Scouting. WSPU also allowed the participating Parliamentarians to broaden their perspective on Scouting and realize its full potential. As a result, WSPU is an important tool that allows World Scouting to inform Parliamentarians of Scouting's current agenda. When Parliamentarians return to their home countries, they are better equipped to draft youth policies that are beneficial to the youth movement in general and Scouting in particular. Furthermore, as a consequence of WSPU, awareness of Scouting's involvement in issues like peace, environment and health, has increased not only on a national level but a global one as well.
WSPU enjoys Consultative Status with the World Scout Committee.
For more information about WSPU, please visit their website at wspu.info.

Jumamosi, 8 Juni 2013

SKAUTI WA DAR-ES-SALAAM WAFANYA ZIARA YA UTALII WA NDANI

  • Waenda Mbuga ya Mikumi na Kambi ya Bahati Morogoro

Baadhi ya Skauti wakiwa katika kiwanja cha Makao Makuu ya Skauti Upanga, Dar Es Salaam.

Skauti wa Wilaya ya Temeke, Ilala na Kinondoni kutoka Mkoa wa Dar Es Salaam wanafanya ziara ya Kimafunzo na Utalii wa ndani mkoani Morogoro, ziara hiyo itakuwa ya siku tatu kuanzia tarehe 08 Juni, 2013. Kwa mujibu wa kiongozi wamsafara huo Skauta Heldon Mwaipopo alisema, "Ziara hii ni ya kielimu, utalii na mafunzo kwa skauti vijana wa shule ya msingi kwa lengo la kuwafundisha vijana kwa ualisia mambo mbalimbali ya kitalii katika nchi yetu" Pamoja na hayo Skauti hao watapata fursa nzuri ya kutembelea mbuga ya wanyama ya Mikumi na Milima ya Uruguru mkoani Morogoro. Ndugu Mwaipopo aliendelea kusema "Pia vijana wetu watapata nafasi ya kuona wanayojifunza katika masomo yao na vilevile katika mafunzo ya Skauti ambayo yatawasaidia kiafya na kuwajengea uwezo wao wa kufikiri na kutenda vyema katika masomo yao ya darasani na maisha yao ya kila siku"
Heldon Mwaipopo Kiongozi wa ziara
Skauti 158 wameshiriki katika ziara hiyo ya kielimu na utalii wa ndani.
Pamoja na hayo yote ndugu Mwaipopo aliendelea kusema "Tunashukuru kwa ushirikiano wa walimu, wazazi na walezi kwa kuwakubalia watoto wao katika ziara hii, kuwepo kwa pamoja vijana hawa 158 kutoka katika maeneo tofauti na rika tofauti kiujumla watapata changamoto ya kujadiliana na kubadilishana mawazo jinsi wanavyoishi, na huu ni mpango endelevu tunawakaribisha zaidi vijana na baada ya siku tatu tutakuwa na ziara nyingine tena"

Moja ya basi walilosafiria Skauti kwenda Morogoro
Katika ziara hiyo ambayo ilikuwa na mabasi madogo aina ya Toyota Coaster sita, skauti watapata nafasi ya kutembelea kambi ya kitaifa ya Bahati (Bahati Camp), Mbuga ya wanyama ya Mikumi na Milima ya Uruguru kuanzia tarehe 08 mpaka 11 Juni 2013. Mwalimu Mwinuka kutoka shule ya msingi ya Kisukulu alisema "Ziara hii tumeiandaa rasmi kwa ajili ya utalii wa ndani ambayo itawasaidia watoto kubadilisha mazingira na hasa kimasomo kuangalia mbuga na wanyama na kujifunza aina mbalimbali ya wanyama, ndege na pia kuangalia milima na uoto wa asili wa sehemu furani na nyingine tofauti yake nini itasaidia watoto kuelewa masomo yao na pale linapokuja swali la mazingira, ndege na wanyama watakuwa tayari wameona na kuelezewa hali halisi. Na sisi kama Skauti tutakuwa tayari kuelezea jamii kuhusu utalii wa ndani na kuwafanya wageni kutembelea kwani nasi tumevutiwa sana"
Baadhi ya wanafunzi wanaoshiriki mafunzo hayo walielezea furaha yao ya kupata nafasi hii. Mtoto Salim Hassani na Selemani Sudi toka shule ya Msingi Rutihinda walionyesha furaha yao juu ya safari hiyo ambayo kwa upande wa shule hiyo waliongozwa na Mwalimu Kilindo Johnson.
Kamishna Peter Paul
Kamishna wa Skauti Mkoa wa Dar Es Salaam alisema "Safari hii ni Mafunzo ya Skauti, kimsingi ni sehemu moja ya mipango ya Skauti ambazo lazima zifanywe ili kuonyesha kuwa Skauti hipo na hii ni sehemu mojawapo ya mipango ya makundi" 
Katika hatua nyingine Kamishna Msaidizi wa Skauti Wilaya ya Ilala anafuatilia kwa karibu ziara hii katika hatua ya kuakikisha kuwa ratiba na mipango hiyo inafuatwa kama ilivyopangwa, zaidi Kamishna Peter Paul alisema "Mimi nitaondoka na usafiri tofauti katika kufuatilia nidhamu ya Skauti inafuatwa kwa mujibu wa ahadi na kanuni zetu"

Jumanne, 4 Juni 2013

KUELEKEA KUAPISHWA KWA SKAUTI MKUU

  • Chama cha Skauti kina mengi ya kurekebisha

    Mlezi wa Skauti Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete (Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania)
    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mlezi wa Skauti Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kumwapisha Skauti Mkuu mteule ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mh. Mwantum Mahiza, taarifa iliyotufikia kutoka kwa mtoa taarifa wetu inasema, tarehe 19 Juni, 2013 Skauti Mkuu mteule ataapishwa na kufuatiwa na shamra shamra katika viwanja vya Karimjee siku hiyo hiyo. 
    Katika hatua nyingine Skauti Mkuu atakutana na changamoto nyingi za migogoro ndani ya Chama cha Skauti Tanzania. Baadhi yake ni pamoja na migogoro ya umiliki wa ardhi ambao unawahusu wadhamini wa chama katika kesi namba 185/2004 katika Mahakama Kuu ya Tanzania, katka kesi hii inasadikiwa waliokuwa viongozi miaka ya 2003 waliingia mikataba isiyofuata taratibu kwa mujibu wa katiba ya chama cha Skauti Tanzania. Kwa upande wa kesi hii ambayo iliyochukua muda mrefu sana, Chama cha Skauti kimeshindwa kutafuta suruhisho nje ya Mahakama hii inatokana na baadhi ya viongozi wa Skauti kutoifuatilia, athali yake itapelekea wadhamini wa Chama cha Skauti kupandishwa Mahakamani. Kesi hii itasikilizwa tena tarehe 06 Juni, 2013 katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

    Mh. Mwantum Mahiza Skauti Mkuu Mteule (Mkuu wa Mkoa wa Pwani)
    Kwa upande mwingine, kesi ya kukamatwa na kutaka kuuzwa kwa jengo la chama cha Skauti ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa hukumu ya Mahakama kuu ya Kazi Tanzania ni madai ya msingi ya Bi. Agnes George. Katika kesi hii yenye namba 175/2009, Chama cha Skauti kikiwa na dai moja wapo la msingi kuwa Bi. Agnes anakidai chama kiasi cha Tsh 5,300,385.60 na kwa upande wa mdai ana hoja yake ya msingi ya madai ya Tsh 111,510,384.60. Ikumbukwe pia katika kesi hii ilikwisha kipelekea Chama kukamatwa na kuuzwa kwa gari aina ya Suzuki - Vitara ikiwa kama fidia ya mdaiwa. Kesi hii imepangwa kusikilizwa tarehe 20 Juni, 2013 katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

    Mbali na matatizo au chanagamoto hizo ambazo Skauti Mkuu na uongozi wake unaotarajiwa unahitaji kuzimaliza kwa haraka zaidi ukizingatia ni za muda mrefu. Pia chama kimepoteza mvuto kwa jamii na kuwa na makundi, mikataba isiyokuwa na tija, karakana ya kutengenezea magari (Garage), sehemu ya kuuzia vileo (Bar) na ujenzi holela katika eneo la makao makuu ya Skauti ambayo upelekea kuchafua sura na mandhari ya eneo.