Jumatatu, 27 Mei 2013

Mafunzo ya PTC na Wood Badge

Kamishna Abubakari Mtitu
Chama cha Skauti Mkoa wa Dar Es Salaam kimeandaa mafunzo ya awali ya uongozi kwa Skauti. Hii ni fursa kwa Skauti kuanzia miaka ya 18 na kuendelea kupata mafunzo hayo.

Kwa mujibu wa Kamishna Skauti mkoa wa Dar Es Salaam, Kamishna Abubakari Mtitu alisema, Mafunzo hayo ni fursa kwa watu wazima kujifunza Skauti na ata wale walio mikoa mingine wanakaribishwa kushiriki mafunzo.
Kamishna Mtitu aliongeza kusema, "Tumeandaa fursa nyingine ya mafunzo ya watu wazima katika ngazi ya Wood Badge ili tuweze kupata watu wazima watakaoweza kusimamia shughuli za Skauti katika ngazi mbalimbali".

Kwa wale watakaopenda kushiriki mafunzo hayo, fomu za ushiriki zinapatikana sasa, tafadhali pakua fomu hizo kwa kubonyeza hapa; http://www.facebook.com/groups/171718552973513/

Hakuna maoni: