Jumamosi, 29 Julai 2023

SKAUTI WANAOSHIRIKI JAMBOREE YA 25 WAAGWA RASMI

 Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia na Rais wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe Profesa Adolf Mkenda  mara baada ya kufika makao makuu ya chama cha skauti yaliyopo upanga jijini dar es salaam leo julai 28,2023  katika hafla fupi ya kuwaaga skauti  wanaokwenda Nchini Korea kwenye kusanyiko la 25  la skauti duniani(25th World Scout  Jamboree ).

Mhe profesa Adolf Mkenda amewaasa vijana wanaokwenda Nchini Korea kuipeperusha vyema Bendera ya Taifa na kutangaza vivutio vya utalii vya Nchini Tanzania wanapofika huko, Mhe Profesa Mkenda Pia Amepokea mfano wa bima kwa ajili ya safari itakayosaidia skauti hao pindi wawapo safarini wafikapo na kurudi.

Hafla hii ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama cha Skauti Tanzania akiwemo Skauti Mkuu Alt Mhe Rashid Kassim Mchatta,Naibu Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Lt Abuubakar Mtitu, Kamishna Mtendaji wa Chama cha Skauti Tanzania Bi Eline Kitaly pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali na Wazazi,Walimu na Skauti. 


MATUKIO KATIKA PICHA 






Chanzo cha Habari Tanzania Scouts Association PR-Lab