Ijumaa, 4 Septemba 2015

MASHINDANO YA SKAUTI MKOA WA DAR ES SALAAM YAANZA RASMI 04 - 06 AGOSTI 2015











Ijumaa, 14 Agosti 2015

RAIS PROF. JAKAYA KIKWETE KUUTUBIA SKAUTI

MKUTANO MKUU WA BARAZA KUU TANZANIA

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE MGENI RASIMI


Wakati Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la Chama cha Skauti Tanzania ukianza kwa semina elekezi kwa Viongozi wote wa Skauti Tanzania.

 Viongozi wa Skauti kutoka pande zote za Mikoa ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani waliwasili kuanzia tarehe 12-08-2015 tayari kwa Mkutano Mkuu wa Baraza kuu la Taifa ambapo utakaofanyika siku ya jumamosi, tarehe 15-08-2015 katika Ukumbi wa Karimjee Dar Es Salaam, ambapo Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa Professor Jakaya Mrisho Kikwete atakuwa mgeni rasimi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pia ni Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania Prof. Jakaya Kikwete

Pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwepo pia watakuwepo viongozi wa Chama cha Skauti Tanzania, rais wa Chama cha Skauti Tanzania Dkt. Shukuru Kawamba (waziri wa Elimu na Ufundi), Skauti Mkuu Mheshimiwa Mwantum Mahiza (Mkuu wa Mkoa wa Lindi), Kamishna Mkuu Mheshimiwa Abdulkarim Shah (Mbuge wa Mafia - anayemalizia muda wake), Naibu Kamishna Mkuu Ndugu Rashid Mchatta, Mwenyekiti wa Kamati Tendaji Balozi Nicholaus Kuhanga, pamoja na Ma-kamishna wote wa Mikoa na Wilaya wa Skauti Tanzania.

Katika mkutano huo ambapo Rais J. Kikwete atachukua nafasi ya kuwaaga Skauti Tanzania, wito umetolewa kwa wadau na marafiki wa Skauti kujumuika kwa pamoja katika tukio hilo linalotarajiwa kuanza saa 2 asubuhi ya tarehe 15-08-2015, Jumamosi katika Ukumbi wa Karimjee Dar Es Salaam.

Sambaza Upendo

Jumanne, 4 Agosti 2015

MKUTANO MKUU WA BARAZA KUU TANZANIA

 






SAMBAZA UPENDO
Mtandao wa Skauti Mkubwa na Mpana Tanzania

Ijumaa, 12 Juni 2015

MZEE NGUNGA AFARIKI DUNIA

PENGO LAKE HALITAZIBIKA

NI VETERANI SKAUTI ALIYEKABIDHIWA SKAUTI NA WAKOLONI


Chama cha Skauti Tanzania (TSA) kimepatwa na pigo lingine la kuondokewa na kipenzi chake aliyeanza Skauti tangu enzi ya Ukoloni.

Marehemu Ndugu Isdor Stanslaus Ngunga alizaliwa tarehe 12 Januari 1928 katika kijiji cha Mwenge Mshindo, Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na alijiunga katika Chama cha Skauti Tanzania Mkoa wa Ruvuma mwaka 1940 akiwa ni mwanafunzi katika shule ya Mtakatifu Benedict (Father Benedict Middle School) iliyopo Peramiho Mkoani Ruvuma.

Marehemu Mzee Isdor Stanslaus Ngunga, enzi ya uhai wake akiwa nyumbani kwake alipotembelewa na waandishi wa Dar Scout Media kwa mahojiano.

Marehemu alipenda sana mafunzo ya Skauti na kuendelea nayo hadi alipojiunga na Elimu ya juu katika Chuo hicho hicho cha Mtakatifu Benedict, Peramiho.

Marehemu Mzee Ngunga alipata mafunzo mbalimbali ya Skauti ndani na nje ya nchi. 

  • Alipata Mafunzo ya Mwanzo ya Uongozi (PTC) mwaka 1950
  • Mafunzo ya Skauti (Wood Badge - WB) mwaka 1955.

UONGOZI

Amewai kushika nafasi mbali mbali za uongozi ambapo mwaka 1955 aliteuliwa kuwa Kiongozi wa Skauti, yaani "Scout Master" wa kundi la Skauti la Litembo mjini Songea.
  • Mwaka 1960 aliteuliwa kuwa Kiongozi wa Skauti wa Wilaya (District Scout Master) katika Wilaya ya Songea.
  • Mwaka 1961 aliteuliwa kuwa "Field Commissioner" Makao Makuu ya Chama cha Skauti Tanzania.
  • Mwaka 1979 aliteuliwa kuwa Kamishna Mkuu Msaidizi wa Mafunzo Tanzania.
  • Mwaka 1994 aliteuliwa kuwa Kamishna Mkuu Msaidizi Mambo ya Nje.
  • Mwaka 1992 aliteuliwa kuwa Naibu Kamishna Mkuu Tanzania.
  • Mwaka 1998 aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mafunzo katika Chama cha Skauti Tanzania.
  • Mwaka 2008 hadi mauti yake aliteuliwa kuwa Mshauri wa Chama cha Skauti Tanzania.

Skauti wakiwa wamebeba sanduku la mwili wa Marehemu Mzee Ngunga kutoka nyumbani kwake Kijitonyama barabara ya Akachube kuelekea Kanisani kwa maombi, tarehe 17 Juni 2015 siku ya Jumatano.
Marehemu Ndugu Isidori Ngunga katika shughuli zake za kazi kama Mwalimu katika Chuo cha Ualimu Peramiho na baadae Nangosho Mbambabay, Seminary ya Kigonsera, Litembo na Mtyangimbole huko Ruvuma aliendelea na shughuli za Skauti, shughuli ambazo alizipenda na pia alifurahi kuona wanafunzi wake wengi wakijiunga na Chama cha Skauti.

KUTOKA WIZARANI HADI SKAUTI

Akiwa ni Mtumishi wa Wizara ya Elimu mara baada ya Nchi yetu kupata Uhuru mwaka 1961, Marehemu Ndugu Isidori Stanslaus Ngunga aliazimwa kutoka Wizara ya Elimu na kufanya kazi kama Field Commissioner katika Chama cha Skauti Tanzania Makao Makuu, kazi ambazo zilimlazimu kusafiri ndani na nje ya nchi, alifanya shughuli za Skauti katika mikoa ya Shinyanga, Dar es Salaam na baadae Lagoni nchini Nigeria.

Kati ya mwaka 1975 hadi 1978 Marehemu Ndugu Isidori Ngunga aliteuliwa na Wizara ya Elimu kuwafundisha  Wakufunzi wa Umoja wa Vijana wa TANU/CCM mafunzo ya Ujasiri na Maarifa na kuwafanya wawe wakakamavu kama vijana wa Skauti.

Marehemu Isidori Ngunga (aliyevaa sare ya Skauti) enzi ya uhai wake katika picha ya pamoja na baadhi ya wajukuu na watoto wake, picha hii alipigwa Juni 14, 2014 alipotembelewa na Dar Scout Habari kwa mahojiano ya kuweka kumbukumbu za Skauti.

Mwaka 1974 hadi 1993 Marehemu Ndugu Isidori Stanslaus Ngunga katika kutimiza majukumu yake ya kikazi kama Mwalimu katika shule za Sekondari Jangwani na Mtakatifu Anthony zote za Jijini Dar Es Salaam aliendelea na Skauti kwa wakati huo akiwa ni Mshauri na Mkufunzi wa Chama cha Skauti Tanzania Makao Makuu.

Marehemu Ndugu Isidori Stanslaus Ngunga atakumbukwa daima na Uongozi wa Skauti na Ma-Skauti ndani na nje ya nchi kutokana utendaji wake mahiri na usimamizi mzuri wa Program za vijana na viongozi wa Skauti kwa ujumla.

Aidha Marehemu Ndugu Isidori Stanslaus Ngunga alishiriki kikamilifu katika shughuli ya marekebisho ya Katiba mpya ya Chama cha Skauti Tanzania, Katiba ambayo hadi hivi sasa bado ipo katika hatua za mwisho.

Baadhi ya Skauti wakiwa katika kaburi la Marehemu Mzee Ngunga wakiimba nyimbo ya Skauti baada ya mazishi ya Mzee Isdor Ngunga katik makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam, tarehe 17 Juni 2015 Siku ya Jumatano.

Baadhi ya Skauti wakiwa katika maombi katika kaburi la Marehemu Mzee Isidori Ngunga.
Kamishna Mtendaji Ndugu Eline Kitaly kwa niaba ya Skauti Mkuu na Ma-Skauti wote Tanzania akisoma wasifu wanVeterani Marehemu Isidori Stanslaus Ngunga katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dar Es Salaam baada ya mazishi. Tarehe 14 Juni 2015, siku ya Jumatano.

Skauti wakiwasha mishumaa katika kaburi la Marehemu Ngunga


Marehemu Ndugu Isidori Stanslaus Ngunga alikuwa Mtunzi na Mwandishi wa Vijarida mbalimbali vya Mafunzo ya Skauti na kama Chama tunaahidi kuendeleza pale alipoishia.

Chama cha Skauti Tanzania tutamkumbuka daima Marehemu Veterani, Skauta, Mkufunzi na Mshauri wa Chama cha Skauti Tanzania ambaye ametutoka ghafla, pengo ambalo litachukua muda mrefu kuzibika.

Chama cha Skauti Tanzania tumempoteza Kiongozi mahiri, hodari, Shupavu na Mchapakazi, ambaye tutamkumbuka na kuenzi jina lake daima.

Sisi sote tulimpenda, lakini MUNGU amempenda zaidi.


Viongozi wa Skauti mbalimbali walikuwepo katika mazishi ya Marehemu Mzee Isidori Ngunga

Padri akiongoza misa ya kumuombea Marehemu Mzee Ngunga, Kanisani RC Mwananyamala.



Skauta Kiluswa akitoa heshima yake ya mwisho kwa Marehemu Mzee Ngunga, nyumbani kwa marehemu Kijitonyama, Jijini Dar Es Salaam.



Kamishna Mtendaji Ndugu Eline Kitaly akitoa heshima yake ya mwisho kwa Marehemu Mzee Ngunga, nyumbani kwa marehemu Kijitonyama, Jijini Dar Es Salaam.

Mwenyekiti wa Kamati Tendaji (TSA) Barozi Nicolaus Kuhanga (aliye vaa shati la kitenge) akifarijiana na Makamo Mwenyekiti Kamati Tendaji Mzee Mwaking'inda (aliye vaa shuti) wakati wa mazishi ya Marehemu Mzee Ngunga katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar Es Salaam. 


BURIANI Prof. Isidori Stanslaus Ngunga

12-01-1928 --- 07-06-2015














TUNAMUOMBA MWENYEZI MUNGU AIPUMZISHE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI.

AMEEN.





Habari hii kwa msaada wa Chama cha Skauti Tanzania
Kwa habari zaidi ya mahojiano ya Marehemu Ndugu Isdor Stanslaus Ngunga na Dar Scout Habari, yaliyofanyika 14 Julai 2014, picha na habari za Viongozi wa Skauti, Skauti na chimbuko pamoja sababu ya Marehemu Ngunga kuuitwa Professor wa Skauti Tanzania. Tembelea ukurasa huu tarehe 21 Juni 2015.

(c) Dar Scout Media, Scout Chat Forum 2015

Jumapili, 29 Machi 2015

SKAUTI WAPO KATIKA MAJONZI MAKUBWA

MHOMWA HATUNAYE TENA


Chama cha Skauti Tanzania kimepatwa na pigo kubwa baada ya kufariki aliyekuwa Kamishna Mkuu ndugu Lawrence Humphrey Mhomwa.

Enzi ya uhai wake Marehemu Lawrence Hamphrey Mhomwa (wa pili kutoka kushoto) akiwa na baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza kuu wakifuatilia jambo kwa makini, ulifanyika tarehe 05 Januari 2013 katika ukumbi wa Don Bosco Upanga
Dar Es Salaam.

Kwa mujibu wa msemaji wa wana-familia ya marehemu Mhomwa alisema, "Mpendwa Lawrence alifariki tarehe 20.03.2015"

Marehemu Lawrence Mhomwa, mpaka anafariki alikuwa mfanyakazi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATC).

Marehemu ndugu Lawrence Hamphrey Mhomwa alizaliwa katika kijiji cha Ng'ombo Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma tarehe 18 Desemba 1958.

Marehemu Lawrence aliamia jijini Dar Es Salaam na kuishi na mjomba wake ndugu Gabriel Matao na kuanza Elimu ya Msingi katika Shule ya Uhuru Mchanganyiko mwaka 1967 hadi mwaka 1974 alipofaulu na kujiunga na Shule ya Sekondari ya Azania mwaka 1975 hadi 1978.

Skauti kikosi maalum cha pared wamebeba sanduku lenye mwili wa marehemu Lawrence Humphrey Mhomwa kuelekea kanisani kwa ibada.

Kamishna Mkuu wa Skauti Mhe. Abdulkarim Shah (Mb) alimuelezea marehemu Mhomwa alikuwa mtu shupavu na alikuwa kiongozi pamoja na mkufunzi wake katika nishani mbalimbali za Skauti alizopata Mhe. Shah, pia Kamishna Mkuu Mhe. Shah aliendelea kusema, " marehemu ndungu Lawrence Mhomwa alijiunga na Chama cha Skauti Tanzania mkoa wa Dar Es Salaam tangu alipokuwa katika shule ya Msing ya uhuru Mchanganyiko miaka ya 1970 na kuendelea na shughuli  za Skauti hadi alipoingia katika shule ya Sekondari ya Azania mwaka 1975.

Kamishna Mkuu Mhe. Shah (Mb) aliendelea kusema, " Akiwa shuleni Azania Marehemu Lawrence Mhomwa aliongeza juhusi na maarifa zaidi katika shughuli za Skauti na kutunikiwa nishani ya Kwanza ya Skauti (First Class) tarehe 03.09.1975, ambapo pia alichaguliwa kuwa kiongozi wa Kikosi (Patrol Leader), na baadae kuwa kiongozi wa kikundi (Troop Leader).

Skauti Mkuu Mhe. Mwantum Mahiza (Mkuu wa Mkoa wa Lindi) akisalimiana na Skauti alipowasili katika nyumba ya msiba wa Marehemu Lawrence Humphrey Mhomwa, tarehe 23.03.2015 Kinondoni Studio  jijini Dar Es Salaam.
Mhe. Shah (Mb) alizidi kufafanua kuhusu marehemu Lawrence Mhomwa kuwa, baada ya kumaliza Elimu yake ya Sekondari katika Shule ya Azania na huku akifanya kazi, Marehemu Lawrence Mhomwa aliendelea na shughuli za Skauti hadi kuteuliwa kuwa Kamishna wa Skauti Wilaya ya Kinondoni mwaka 1980 hadi 1985.

Marehemu Lawrence Mhomwa alishika nyadhifa mbali mbali.
Mwaka 1986 hadi 1990 alikuwa Kamishna wa Skauti Mkoa wa Dar Es Salaam, mwaka 1991 hadi 2001 aliteuliwa kuwa Kamishna Mkuu Msaidizi Mafunzo,. Makao Makuu ya Chama cha Skauti Tanzania.
Mwaka 2002 hadi 2005 aliteuliwa kuwa Kamishna Mkuu Msaidizi Programu za Vijana, makao makuu ya Chama cha Skauti Tanzania na mwaka 2008 hadi 2012 aliteuliwa kuwa Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania ambapo baada ya hapo alimwachia Mhe. Abdulkarim Shah (Mbunge wa Mafia)

Viongozi mbalimbali walihudhuria mazishi ya Marehemu Lawrence Mhomwa, Kamishna Mkuu Mhe. Abdulkarim Shah (wa pili kutoka kulia) akifuatiwa na aliyekuwa Skauti Mkuu ndugu Kipingu (aliyevaa suti wa tatu toka kulia) na Kamishna Mkuu Msaidizi Mambo ya Nje, Uhusiano wa Kimataifa, Mawasiliano na Jota-Joti Skauta Fredirick Peter Nguma (wa pili kutika kushoto)

Marehemu ndugu Lawrence Mhomwa alipata mafunzo mbalimbali ya Skauti ndani na nje ya Nchi, mafunzo ya Ujasiri na Maarifa, ikiwa ni pamoja na kupanda Mlima wa Kilimanjaro akiwa Skauti mwenye umri mdogo.

Marehemu pia ameshiriki katika kambi mbali mbali za Skauti ndani na nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na Jamboree ya Dunia ya Skauti kutimiza miaka 100 iliyofanyika nchini Uingereza mwaka 2007.

Mwaka 1978 alipata Mafunzo ya Mkufunzi Msadizi (ALT) Chama cha Skauti Tanzania katika kambi kuu ya Bahati mkoani Morogoro.

Mwaka 1994 alipata Mafunzo ya Mkufunzi Mkuu (Leader Trainer) kutoka kambi ya Skauti Nyeri, Kenya.

Hadi alipofariki, marehemu Lawrence Humphrey Mhomwa alikuwa Mkufunzi wa Chama cha Skauti Tanzania.

Enzi ya uhai wake, Marehemu Lawrence Humphrey Mhomwa akiwa katika utendaji kazi wa Skauti ofisini kwake Chama cha Skauti Tanzania.

Msemaji wa familia ya marehemu alizungumzia kuhusu marehemu katka shughuli zake za kazi, msemaji huyo alisema, Marehemu ndugu Lawrence Humphrey Mhomwa baada ya kumaliza Elimu yake ya Sekondari aliajiliwa na Hotel ya Kunduchi Beach iliyopo jijini Dar Es Salaam na kufanyakazi kama Mhudumu na baadae kuhamishiwa Idara ya Utunzaji bidhaa (store keeper) mwaka 1978 mwishoni hadi mwanzoni mwaka 1980.

Tarehe 30 Julai 1980 aliajiliwa na Shirika la Ndege la Tanzania (ATC) kama mhudumu wa ndani ya ndege (cabin crew). Mwaka 1986 kutokana na utendaji wake mahiri wa kazi, alipandishwa Cheo kutoka Muhudumu Mkuu (Senior crew hadi kuwa Senior Fight Pursers).

Marehemu Lawrence Mhomwa alifanyakazi katika Idara mbalimbali ndani ya Shirika la ndege la Tanzania, ikiwa ni pamoja na Idara ya Mizigo (Cargo Department) pamoja na Idara Uendeshaji (Operation Department) mwaka 1990.

Aliendelea kusema kuwa, "Marehemu Lawrence Mhomwa alipata mafunzo mbalimbali kuhusu masuala ya Usafiri wa ndege na usalama ndani ya ndege. Mafunzo hayo pamoja na mengine ambayo yalimwezesha marehemu ndugu Lawrence Mhomwa kupandishwa cheo na kuwa Mkufunzi Mkuu (Chief Instructor) kutoka chuo cha Wahudumu wa ndege cha Shirika la Ndege la Tanzania.

Skauti mbali mbali waliudhuria maziko ya Marehemu Lawrence Humphrey Mhomwa kama wanavyoonekana katika picha wakiwa katika eneo la makaburi ya Kinondoni.

Viongozi wa Skauti wakiwa katika eneo la makaburi ya Kinondoni, kwa ajili ya mazishi ya ndugu Lawrence Mhomwa tarehe 23 Machi 2015. Kamishna wa Mkoa wa Dar Es Salaam ndugu Abubakar mtitu (aliyeshika mwamvuli) na Kamishna wa Wilaya ya Ilala ndugu Crispin .W. Majiya (wa kwanza kushoto) 

Msemaji kwa niaba ya wafanyakazi wenzake wa Shirika la Ndege la Tanzania, alimuelezea marehemu Lawrence Mhomwa kuwa, "Alikuwa mtu mahili sana, na kutokana umahili wake na mafunzo thabiti aliyoyapata kutoka katika Chama cha Skauti Tanzania pamoja na Shirika la Ndege la Tanzania, tarehe 13 Februari 1988 wakati ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania aina ya Boeing 737 ilipotekwa ikiwa safarini kutoka Dar Es Salaam kwenda Kilimanjaro, marehemu ndugu Lawrence Mhomwa ambaye alikuwa ndani ya ndege hiyo kwa siku hiyo, alifanya kazi kubwa sana ya kuwatuliza abiria walikuwa wanataka kupambana na watekeji wa ndege hiyo".

Msemaji huyo aliendelea zaidi kusema, "Kutokana na ushupavu na ujasiri wake huo, tarehe 26 Aprili 1989 katika sherehe za Muungano alitunukiwa NISHANI YA JUU YA USHUPAVU, na Rais wa awamu ya pili Mheshimiwa ndugu Ali Hassan Mwinyi, katika viwanja vya Ikulu jijini Dar Es Salaam". 

Kwa maelezo mengine ambayo Dar Scout Media iliyapata kutoka kwa msemaji wa familia ya marehemu Lawrence Mhomwa kuwa, Marehemu Lawrence Mhomwa pia aliwai kuwa Katibu wa Chama cha Wafanyakazi (COTWU) tawi la Uwanja wa Ndege wa Dar Es Salaam mwaka 2005 hadi 2011 na baade kuendele kuwa mmoja wa Wajumbe wa Chama hicho.

Pia, wahudumu wa ndani ya ndege wa Shirika la Ndege la Tanzania, walimuelezea marehemu Lawrence kuwa alikuwa mtu wa watu na wa kuigwa hakika watamkosa wa kuweza kumlinganisha.

Hadi alipofariki tarehe 20 Machi 2015Marehemu Lawrence Humphrey Mhomwa alikuwa anashikiria wadhifa wa Mkufunzi Mkuu (Chief Instructor) katika Chuo cha Wahudumu wa Ndege wa Shirika la Ndege Tanzania.

TAARIFA ZA UGONJWA HADI KUFARIKI KWAKE

Matatizo ya kuugua kwa marehemu Lawrence Mhomwa yaliaanza kiasi cha wiki nne (4) zilizopita, akisumbuliwa na matatizo ya maumivu katka koo.

Marehemu alikuwa akipata matibabu katika Hospitali ya Regency na TMJ zote za jijini Dar Es Salaam na alikuwa akiendelea vizuri tu hadi usiku wa tarehe 19 Machi 2015 hali yake ilipobadilika ghafla, na asubuhi ya tarehe 20 Machi 2015 marehemu aliomba familia yake impeleke kwa Mchungaji kwa ajili ya maombi, akiwa njiani kuelekea kwa Mchungaji, hali yake ilibadilika tena, na familia kuamua kumpeleka hospitali ya Mwananyamala ambapo alifariki siku hiyo mchana.

Marehemu atakumbukwa daima kwa umahiri wake na utendaji kazi wake. Taasisi hizi mbili za Chama cha Skauti Tanzania na Shirika la Ndege la Tanzania, ambapo muda wote wa maisha yake amekuwa akizitumikia.

Marehemu Lawrence Humphrey Mhomwa ameacha Mjane na watoto wanne (4).


PICHA MBALI MBALI KATIKA MAZISHI YA MAREHEMU LAWRENCE MHOMWA















MWENYEZI MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU LAWRENCE HUMPHREY MHOMWA MAHALA PEMA PEPONI, AMIN.



  • Dar Scout Media
  • Scout Chat
  • +255-655-095559
  • Scout Breaking News
  • +255-755-095559