Ijumaa, 27 Desemba 2013

MASHINDANO YA SKAUTI AFRIKA MASHARIKI NA KATI


  • Timu ya Tanzania yakabidhiwa bendera kuipeperusha Burundi
Kamishina Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mhe. Abdulkarim Shah akiwapa nasaha Timu ya Skauti ya Taifa na baadhi ya Skauti (awapo pichani) kwenda kushiriki mashindano ya Skauti ya Afrika Mashariki na Kati yatakayofanyika nchini Burundi. Kulia ni Naibu Kamishna Mkuu Ndugu Kassim Mchatta na kushoto ni Kamishna Mkuu Msaidizi kitengo cha Jinsia na Mipango ya Vijana (Youth Programme and Gender). Tarehe 26.12.2013 katika kiwanja cha Skauti Makao Makuu Upanga.       

Timu ya Taifa ya Skauti Tanzania imekabidhiwa Bendera ya Taifa na ya Chama cha Skauti Tanzania pamoja na vifaa vyote baada ya kupata mafunzo na mbinu zaidi za Skauti kwenda kushiriki katika mashindano ya Skauti ya Afrika Mashariki na Kati pamoja na kuhudhuria kongamano la Vijana la Skauti nchini Burundi. Timu hiyo inatarajia kuondoka nchini kuelekea Burundi tarehe 29 Desemba 2013 hadi tarehe 04 Januari 2014.

Akikabidhi bendera hizo, Kamishna Mkuu wa Skauti Tanzania Mhe. Shah aliwatakia wawakirishi hao kila la heri na kuwataka Skauti na Watanzania wote kuwaombea mafanikio mema na hatimaye kurudi nyumbani na ushindi. Mheshimiwa Shah alisema, "Ushindi mtakao upata ni wa Tanzania mzima na siyo wa mtu mmoja mmoja, hivyo pamoja na mafunzo na mbinu za Skauti mlizopata, tuna waombea kila lililo la kheri kwa Mwenyezi Mungu mfike salama na mpeperushe vyema bendera ya nchi yetu" aliongeza kwa kusema, "Sisi Skauti na Watanzania wote tupo pamoja nanyi katika safari na katika mashindano hayo, mtuwakirishe vyema"
 
Kamishna Mkuu wa Skauti Tanzania Mheshimiwa Shah akikabidhi bendera ya Skauti Tanzania kwa timu ya Skauti itakayoshiriki mashindano ya Skauti ya Afrika Mashariki na Kati nchini Burundi.

Kamishna Mkuu wa Skauti Tanzania Mheshimiwa Shah akikabidhi bendera ya  Tanzania kwa timu ya Skauti itakayoshiriki mashindano ya Skauti ya Afrika Mashariki na Kati nchini Burundi.
Kamishna Mkuu wa Skauti Tanzania Mheshimiwa Shah (kulia) akiteta jambo na Kaimu Kamishna Mtendaji Ndugu Gerald Mkude (Brigedia Jenerali Mstaafu) katika hafla ya kuwaaga timu ya Skauti ya Taifa katika kiwanja cha Makao Makuu ya Skauti Upanga tarehe 26/12/2013.
Baadhi ya Vijana wa kike wa timu ya Skauti ya Taifa inayokwenda nchini Burundi kwa Mashindano ya Skauti Afrika Mashariki na Kati

Baadhi ya Vijana wa kiume wa timu ya Skauti ya Taifa inayokwenda nchini Burundi kwa Mashindano ya Skauti Afrika Mashariki na Kati

Baadhi ya Vijana wa kiume wa timu ya Skauti ya Taifa inayokwenda nchini Burundi kwa Mashindano ya Skauti Afrika Mashariki na Kati na Kongamano la Vijana la Skauti wakicheza moja ya ngoma ya kimila Tanzania.

Kamishna Mkuu Mheshimiwa Shah (mwenye miwani) katika picha ya pamoja na baadhi ya Skauti na timu ya Skauti ya Taifa inayokwenda nchini Burundi kwa Mashindano ya Skauti Afrika Mashariki na Kati (mtsari mbele wa pili kulia mwenye furana nyeusi ni Naibu Kamishna Mkuu ndugu Kassim Mchatta)
Baadhi ya vijana wa timu ya Skauti ya Taifa wakionyesha jambo katika viwanja vya Makao Makuu ya Skauti Upanga tarehe 26.12.2013

Baadhi ya vijana wa timu ya Skauti ya Taifa wakiteta jambo katika viwanja vya Makao Makuu ya Skauti Upanga tarehe 26.12.2013

Timu ya Skauti ya Taifa itakayoshiriki mashindano ya Skauti nchini Burundi
 

Ijumaa, 22 Novemba 2013

KAMSHINA MKUU ATANGAZA UTEUZI WA MAKAMISHNA WA MIKOA

  • Ndani ya mwezi mmoja wawe wameandaa mapendekezo ya makamishna wa wilaya.

Taarifa kwa vyombo vya habari leo mchana kufuatia kwa Kamishna Mkuu wa Skauti Tanzania MheshimiwaAbdulkarim Shah (Mb) kufanya uteuzi wamakamishna wa mikoa wapya.
Mheshimiwa Abdurkarim Shah (Mb) Kamishna Mkuu wa Skauti Tanzania akitangaza majina ya Makamishna wa Mikoa wapya mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) tarehe 22.11.2013 katika Ofisi za Chama cha Skauti Tanzania, Upanga Dar Es Salaam.

Kufuatia Mkutano Mkuu Maalum wa uchaguzi uliofanyika tarehe 05 Januari 2013, Baraza Kuu la Chama cha Skauti Tanzania lilianzisha hatua za kuwapata viongozi wa chama Kitaifa. Kuanzia wakati huo hadi sasa viongozi mbalimbali wamechaguliwa, wameteuliwa na kuapishwa. Viongozi hao ni pamoja na Skauti Mkuu Mheshimiwa Mwantum Bakari Mahiza (Mkuu wa Mkoa wa Pwani), Mwenyekiti, Makamo Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama Kitaifa.

Katika mtiririko huo wa safu mpya ya viongozi, Kamishna Mkuu Mheshimiwa Abdulkarim E. H. Sahah (Mb) naye alichaguliwa na kuapishwa. Naye kwa mamlaka aliyonayo katika Katiba ya Chama cha Skauti Tanzania aliwateuwa na kuwaapisha Naibu Kamishna Mkuu na Makamishna Wakuu Wasaidizi kumi na wawili (12)

  • UONGOZI MIKOANI NA WILAYANI

 Lengo kuu la chama cha Skauti Tanzania ni kuwatayarisha vijana kwa kuwajenga katika maadili mema ili waweze kuwa waaminifu, wazalendo, rafiki wa wote, watiifu, wachangamfu, waangalifu na kuwa raia safi katika mawazo, maneno na vitendo.
Ili kufikia dhamira hiyo, chama Makao Makuu hakina budi kuueneza na kuusimamia U-Skauti nchini kote. Hili linatekelezwa na kwa Kamishna Mkuu na wawakilishi wake Mikoani na Wilayani.
Kwa mujibu wa Katiba ya Chama cha Skauti Tanzania ya mwaka 1997 Kifungu 6.11 (a) na (b) hawa watamwakilisha Kamishna Mkuu na kuyatekeleza majukumu yao ambayo kimsingi sawa na ya Kamishna Mkuu bali katika himaya zao.  
Kwa mujibu wa Katiba ya Chama cha Skauti Tanzania kifungu 6.5 (e)(vi), Kamishna Mkuu amewateuwa viongozi wa Skauti wafuatao kuwa Makamishna wa Skauti wa Mikoa na wasaidizi wao:-
MKOA: Arusha
Kamishna: Shakirhussein Badruddin
Naibu Kamishna wake: Wilfred James
MKOA: Dar Es Salaam
Kamishna: Abubakari Mtitu
Naibu Kamishna wake: Grace Kado
 
Skauta Abubakar Mtitu alejea tena Kamishna wa Mkoa wa Dar Es Salaam
MKOA:Dodoma
Kamishna: Daktari Swai
Naibu Kamishna wake: Selistine Raphael

MKOA:Geita
Kamishna: Kiracha Nyamsongolo
Naibu Kamishna wake: Marison .S. Gunje
MKOA: Iringa
Kamishna: John Sichone
Naibu Kamishna wake: Lyason Kajembura


MKOA:Kagera
Kamishna: Fr. Process Mutungi
Naibu Kamishna wake: Beda Kyaishozi
MKOA:Katavi
Kamishna: Mrisho Thabiti Kinanda
Naibu Kamishna wake: Selestine Yoachim China
MKOA: Kigoma
Kamishna: Doecles .H. Bigilwa
Naibu Kamishna wake: Eliudi Marwa
MKOA:Kilimanjaro
Kamishna: Hashim Nyari
Naibu Kamishna wake: Habibu .D. Mvungi
MKOA: Lindi
Kamishna: Aloyce Maira
Naibu Kamishna wake: Bakari Kayombo
MKOA: Mara
Kamishna: Yohana Bonyo
Naibu Kamishna wake: Fred Keya
MKOA: Manyara
Kamishna: Basilisa Martin
Naibu Kamishna wake: Khalifa Salehe Mfanya
MKOA: Morogoro
Kamishna: Francis .G. Francis
Naibu Kamishna wake: Mary Mpasa
MKOA: Mtwara
Kamishna: Erasto Nakati
Naibu Kamishna wake: Hassan .M. Mmadi
MKOA: Mbeya
Kamishna: Sadock Ntole
Naibu Kamishna wake: Boniface Dionis
MKOA: Mwanza
Kamishna: Elibarik Mmari
Naibu Kamishna wake: Wande Mwankyara
MKOA:Njombe
Kamishna: Tusiwene Mahenge
Naibu Kamishna wake: Anita Ngole
MKOA: Pwani
Kamishna: Musiba Bebusiba
Naibu Kamishna wake: Esto Joseph Kalale
MKOA: Rukwa
Kamishna: Mohamed Lugoya
Naibu Kamishna wake: Adengula Mwacha
MKOA: Ruvuma
Kamishna: S. .K. Ndunguru
Naibu Kamishna wake: Hamza Basil Bora
MKOA: Simiyu
Kamishna: Kulwa Mtebe
Naibu Kamishna wake: Jumanne Mangoli
MKOA: Shinyanga
Kamishna: Mussa Chama
Naibu Kamishna wake: Peter mgalula
MKOA: Tabora
Kamishna: Erick Nkwera
Naibu Kamishna wake: Kashinde Masamalo
MKOA:Tanga
Kamishna: Lt. Col (Mstaafu) John Mhina
Naibu Kamishna wake: Nassoro Mbajo
MKOA: Singida
Kamishna: Emmanuel Machemba
Naibu Kamishna wake: Juma Sabigoro
 
  • UTENDAJI

Kufuatia uteuzi wa Makamishna hao, taratibu za kuwaapisha na kuwakabidhi waranti na Katiba zitafuata hivi punde. Barua za uteuzi wao zinafuata. Wakati yote haya yanasubiriwa kwa taarifa hii ni ruksa kwao kuanza kazi mara moja. Alisema Mheshimiwa Shah.
  • MAKAMISHNA WA SKAUTI TANZANIA VISIWANI NA WILAYA 

 Kamishna Mkuu mwenye mamlaka ya kuwateua viongozi hawa yupo katika mchakato wa kushauriana na wasaidizi wake. Mara baada ya zoezi hili kukamilika, tangazo rasmi litatolewa.
Mheshimiwa Shah aliendelea kusema, " Kauli mbiu ya Mkutano Mkuu Maalum wa uchaguzi ilikuwa 'UONGOZI IMARA, CHAMA IMARA' alifafanua kuwa, Chama cha Skauti hakina budi kuwa na uongozi imara unaoweza kusimamia maadili ya vijana wetu hapa nchini kuanzia Makao Makuu hadi Vijijini. Ni matarajio ya wadau wote  wa Chama cha Skauti Tanzania kwamba viongozi wote waliochaguliwa, walioteuliwa na watakaoteuliwa wataongoza kwa kuzingatia Katiba na Maadili ya Chama. Aidha wito unatolewa kwa wanachama na marafiki wa Skauti kutoa ushirikiano kwa uongozi uliopo madarakani.
Kamishna Mkuu alimaliza kwa kuwashukuru wanahabari kwa ushirikiano wao.




MKUTANO WA 7 WA MUUNGANO WA WABUNGE SKAUTI DUNIANI

Mwenyekiti wa Umoja wa Skauti Wabunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Abdulkarim Ismail Shah amechaguliwa kuwa Mweka Hazina Mkuu wa Umoja wa Wabunge Skauti wa Dunia (WPSU)

walishiriki katika Mkutano Mkuu wa Sita wa Umoja wa Skauti Wabunge Duniani ambao unajumla ya nchi wanachama zaidi ya 50. Mkutano huo ulifanyika sambamba na uchaguzi wa viongozi wapya, uliofanyika mjini Tokyo Japan kuanzia Novemba Sita hadi Novemba Nane mwaka huu ambapo Tanzania iliwakilishwa na Mheshimiwa Shah na wabunge wengine watano pamoja na Katibu wa Bunge Umoja wa Wabunge Skauti Tanzania ndugu James John Warburg.

Wabunge wengine waliokuwemo kwenye ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo ni Mhe. Gosbert Blandes, Mhe Livingstone Lusinde, Mhe. kuruthum Mchuchuli na Mhe. Lucy Mayenga ambaye ni Makamo Mwenyekiti wa Umoja wa Skauti Wabunge wa Tanzania.

Katika uchaguzi huo ndugu Ryu Shionoya wa Japan amechaguliwa kuwa Rais mpya wa Umoja huo, na makamo wa kwanza wa Rais ni Bi. Ewa thalen Finne kutoka Sweden na makamo wa Rais wa pili ni ndugu Sutham Phanthusak kutoka Thailand.

Akizungumza na wandishi wa habari katikauwanja wa kimataifa wa ndege wa Mwalim Julius Kambarange Nyerere mara baada ya kuwasili kutoka japan, Mheshimiwa Shah amewashukuru wabunge wenzake kwa kumpigiania hadi kushinda kwenye nyadhifa hizo kubwa duniani na kwamba ushindi alioupata ni zawadi kwa Watanzania wote.

Amesema kuchaguliwa kwake kwenye nafasi hiyo ni heshima kwa Tanzania na kwamba ni ushindi kwa Tanzania na kuonyesha kuwa Tanzania inaweza kutoa viongozi katika kuongoza mashirika au taasisi mbalimbali Ulimwenguni, pia mbunge Mvumi Mtera  Mhe. Lusinde alisisitiza kuwa ushindi huo pia umechangiwa na amani iliyopo Tanzania na kwa ushindi huo Tanzania imetangazika katika sekta ya Utalii na kujulikana kijiografia. Aliendelea kusema, "Uchaguzi huo uliohusisha mataifa zaidi ya 50 ulitawaliwa na ushindani mkali, lakini mgombea wa Tanzania alijieleza kwa ufasaha zaidi na vizuri kuwashawishi wajumnbe kumpigia kura na kushinda nafasi hizo.

Mkutano huo mkuu pia ulijadili na kupitisha mabadiliko ya Katiba ambapo muda wa kufanya mkiutano huo umeongezeka kutoka miaka mitatu hadi miaka minne.

Aidha kwamba kuwepo kwenye safu mpya ya uongozi wa Umoja wa Wabunge Skauti wa Dunia utamwezesha kuendeleza vijana kwa kuwapa elimu, ujuzi ili waweze kuajiliriwa au kujiajiri kwa ajili ya maendeleo yao wenyewe na kuondokana na umasikini. Alisema Mhe Shah. 

Mbunge wa Karangwe Mhe. Gosbert Blandes amesema kwamba mkutano huo umemalizika kwa mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kujifunza namna vyama vya Skauti vinavyoendeshwa duniani, ameendelea kusema kuwa 'nchi nyingi duniani wanachukulia Skauti kama chanzo cha elimu na ajira kwa vijana hivyo wao kama wabunge wataishawishi Serikali kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya kusaidia uendeshaji wa shughuli za Skauti nchini.

Wakati huo huo Mkutano wa tisa wa wabunge Skauti duniani unatarajia kufanyika nchini Tanzania katika kipindi cha miaka minne ijayo.

Kikubwa yaliyozungumziwa katika mkutano huo ni:
  • Umuhimu wa kuweka mazingira salama kwa watoto kielimu.
  • Umuhimu wa kuwaandaa na kuwapa fursa vijana kuwa viongozi wa baadaye.
  • Majukumu mbalimbali ambayo Wabunge wanaweza kuyatekeleza kwa ajili ya kuwasaidia vijana na Chama cha Skauti.


Alhamisi, 25 Julai 2013

MAKAMISHNA WAKUU WASAIDIZI WAAPISHWA

  • KAMATI YA UENDESHAJI YAKAMILIKA

Kamishna Mkuu wa Skauti Tanzania Mhe. Abdulkarim Esmail Hassan Shah [MB] (kushoto) akimkabidhi waranti Mkufunzi Skauta Stewart Kiluswa baada ya kumwapisha kuwa Kamishna Mkuu Msaidizi kitengo cha Makao Makuu Hati na Usajili wa Chama cha Skauti Tanzania, tarehe 24 Julai, 2013 katika Ukumbi wa Skauti Makao Makuu Upanga, jijini Dar Es Salaam.

Chama cha Skauti Tanzania kinazidi kukamilisha safu ya juu ya uongozi, Kamishna Mkuu Mhe. Shah (MB) tarehe 19 Julai 2013 alimwapisha Naibu Kamishna Mkuu Skauta Rashid Kassim Mchatta. Katika Kamati ya Uendeshaji hii mpya ambayo wapo waliorudi katika kamati na wengine wapya, pia wapo waliokuwa Makamishna wa Wilaya. Kati ya Makamishna Wakuu Wasaidizi kumi na moja wapya, watano walikuwepo katika kamati iliyoisha muda wake na sita ni wapya. 

Kwa mujibu wa Katiba ya Chama cha Skauti Tanzania, ya mwaka 1997 kifungu 6.5 (e) (vi) Kamishna Mkuu wa Skauti Tanzania amewateuwa na kuwaapisha Makamishna Wakuu Wasaidizi wa Chama cha Skauti Tanzania. Makamishna Wakuu Wasaidizi hao 11 ni katika kukamilisha Kamati ya Uendeshaji katika Chama cha Skauti Tanzania, na kushughulikia vitengo vya, Utawala Bora, Makao Makuu Hati na Usajili, Mafunzo na Rasilimali Watu, Maafa, Majanga na Uokoaji, Jinsia na Mipango ya Vijana, Makambi, Miradi na Maendeleo, Program za Skauti wa Kiislam, Program za Skauti wa Kikristo, Utunzaji na Mazingira, Kazi Maalum na Mambo ya Nje, Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Jota Joti (International Affairs and Jota Joti).
Askofu Gervas Nyaisonga aliteuliwa kuwa Kamishna Mkuu Msaidizi anayeshughulikia kitengo cha Program za Skauti wa Kikristo, ambaye alikuwepo katika Kamati iliyoisha muda wake na kuteuliwa kuendelea na nafasi hiyo tena, hakuwepo katika uapisho huo kwasababu za kikazi ambapo anategemewa kuapishwa siku zijazo hivi karibuni.


Mkufunzi John Lusunike

 Mkufunzi wa Skauti, Skauta John Lusunike
Kamishna Mkuu Msaidizi atakayeshughulikia Utawala Bora (Good Governance), yeye ni Kamishna Mkuu Msaidizi mpya kushika nafasi hii katika Kamati ya Uendeshaji.








Mkufunzi Omari Mavura
Mkufunzi wa Skauti, Alhaj Omari Mavura alishawai kuwa Kamishna Mkuu Msaidizi anayeshughulikia kitengo cha Mipango ya Vijana (Youth Program), Hati na Usajili (Warrant and Registration), Maafa, Majanga na Uokoaji (Risk Management and Disaster) na Jota/Joti ambaye kwa sasa anashughulikia kitengo cha Program za
Skauti wa Kiislam (Muslim Scouts Program)



Faustin Magige



Skauta Faustin Magige alikuwepo katika Kamati ya Uendeshaji iliyoisha muda wake ambapo alikuwa Naibu Kamishna Mkuu, kwa sasa anashughulikia kitengo cha Kazi Maalum (Special Duty).







Egnetha Manjoli


Skauta  Egnetha Manjoli, ni mmoja kati ya wapya katika Kamati hii na anashughulikia kitengo cha Makambi na Kazi za nje (Campsite and Outreach) 









Fredrick .P. Nguma

Skauta Fredrick Peter Nguma, amerudi tena katika nafasi ya kitengo cha Mambo ya Nje, Teknolojia, Habari, Mawasiliano na Jota Joti (International Affairs). Kitengo hiki kimeunganishwa na kitengo cha zamani cha Mawasiliano na Jota Joti ambacho alikuwa anakishughulikia Skauta Hidan Ricco

 
Juma Massudi

Skauta Juma Massudi alikuwepo katika kamati iliyoisha muda wake akishughulikia kitengo cha Hati na Usajili (Warrant and Registration), kwa sasa anashughulikia kitengo cha Maafa, Majanga na Uokoaji (Risk Management and Disaster)







Mkufunzi Stewart Kiluswa
Mkufunzi wa Skauti, Skauta Stewart Kiluswa ni miongoni ya wapya Makamishna Wakuu Wasaidizi katika Kamati ya Uendeshaji, anashughulikia kitengo cha  Makao Makuu Hati na Usajili (HQ Warrant and Registration)








 
Hamis Kerenge Masasa
 Skauta Hamis Kerenge Masasa kabla ya uteuzi wake huu mpya alikuwa Kamishna wa Skauti wa Mkoa wa Pwani, kwa sasa ni Kamishna Mkuu Msaidizi kitengo cha Miradi na Maendeleo (Project and Development)


Mkufunzi Abdallah Sakasa
Mkufunzi wa Skauti Abdallah Sakasa katika historia ya Chama cha Skauti Tanzania alishawai kuwa Kaimu Kamishna Mkuu na Katibu wa Kamati ya Mpito ambayo iliteuliwa na Rais wa Chama cha Skauti ambaye ni Waziri wa Elimu Dkt. Shukuru Kawambwa. Kwa sasa ameteuliwa kushika nafasi ya Kamishna Mkuu Msaidizi anayeshughulikia kitengo cha Rasilimali Watu na Mafunzo (Adult Resource and Training)



Mkufunzi Mary Anyitike
Mkufunzi Skauta Mary Anyitike ni mmoja wapo waliokuwa katika Kamati iliyoisha muda wake, katika historia ya Chama inaonyesha kuwa alishawai kuwa Kamishna Mkuu Msaidizi kitengo cha Mipango ya Vijana (Youth Program) na kitengo cha Rasilimali Watu na Mafunzo (Adult Resource and Training) na sasa amerudi tena nafasi ya
Jinsia na Mipango ya Vijana (Youth Program and Gender)


Amina Maulidi 
Skauta Amina Maulidi aliyekuwa Kamishna wa Skauti wa Wilaya ya Ilala, ameteuliwa kushika nafasi ya Kamishina Mkuu Msaidizi anayeshughulikia kitengo cha Utunzaji na Mazingira (Environment and Conservation)  






Pamoja na kuwaapisha Makamishna Wakuu Wasaidizi hao, Kamishna Mkuu Mhe. Shah (MB) aliwaasa Skauti wote kufanyakazi kwa weledi na moyo wa kujitolea katika kuleta maendeleo ya Chama, pia kuvunja makundi na kutokuwa na maneno ya pembeni, fitina na hatimaye kukipaka matope Chama cha Skauti Tanzania, Mhe. Shah alisema "Sitokubali kuchafuliwa mimi binafsi, Mlezi wa Chama, Rais wa Chama, Skauti Mkuu, Wadhamini wa Chama, Naibu Kamishna Mkuu, Makamishna Wakuu Wasaidizi, Skauti wenzangu na yeyote atakaye kiuka taratibu za Chama cha Skauti hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake"

Kamishna Mkuu Mhe. Abdulkarim Shah (Mb) (wanne kutoka kushoto) katika picha ya pamoja na Makamishna Wakuu Wasaidizi na baadhi ya viongozi wa Skauti nje ya Makao Makuu ya Chama cha Skauti Upanga jijini Dar Es Salaam tarehe 24 Julai, 2013. Baada ya kuwaapisha Makamishna Wakuu Wasaidizi.