Jumanne, 16 Januari 2018

SKAUTI DAR WATOA FOMU

Chama cha Skauti Mkoa wa Dar es Salaam, kimetangaza kuwepo kwa Mkutano Mkuu Maalum unaotarajiwa kuwepo tarehe za mwisho wa mwezi huu wa Januari 2018.
Akihojiwa ofisini kwake jana 15 Januari 2018 ndugu Abubakar Mtitu Kamishna wa Skauti wa Mkoa wa Dar es Salaam alisema, "Mkoa unatarajia kuwepo na Mkutano Mkuu Maalum ambapo tutaunda Bodi ya Skauti Mkoa pamoja na kuchagua Viongozi wapya wa bodi hiyo"

Nafasi zilizotangazwa kugombea ni Mwenyekiti, Makamo Mwenyekiti ambao watakuwa wawili pamoja na wajumbe wa bodi.

 
Tarehe rasmi ya uchaguzi itatangazwa hivi karibu.
Waweza kujaza fomu hizo za kugombea uongozi kwa njia ya kielektroniki (Online) kwa kubonfya hapa https://tzcentenary2017.wordpress.com/2018/01/16/fomu-ya-uongozi-mkoa-wa-dar-es-salaam/ 

Na kwa habari zaidi za uchaguzi wa Skauti Tanzania kwa ngazi ya Taifa tembelea au bonfya hapa https://tzcentenary2017.wordpress.com

 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni