Jumamosi, 6 Januari 2018

HURU KUGOMBEA SKAUTI MKUU

Mchakato wa Skauti Mkuu waanza


Chama cha Skauti Tanzania kimetangaza upatikanaji wa fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, hii ni desturi ya upatikanaji wa uongozi wa Skauti Tanzania.

Kwa kupitia Mkutano Mkuu Maalum wa Baraza Kuu la Chama cha Skauti Tanzania, ambao ndicho chombo ambacho kinapiga kura na kupata majina 3 yatakayopelekwa kwa Mlezi wa Skauti Tanzania ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuteua Skauti Mkuu.

"Kwa sasa inatarajiwa kuwepo kwa uchaguzi mkuu ambapo tarehe rasmi na eneo litatangazwa" alisema Kamishna Mtendaji wa Skauti Bi. Eline Kitaly

 Kwa sasa Skauti Mkuu wa Skauti ni Bi. Mwantum Mahiza, Kamishna Mkuu wa Skauti ni Ndugu Abdulkarim Shah.

Chama cha Skauti pamoja na kuwa na Makamishna wakuu wa saidizi pia kuna Naibu Kamishna Mkuu ambaye ni ndugu Rashid Mchatta, viongozi wote hao wanamaliza muda wao wa uchaguzi baada ya kupatikana viongozi wapya baada ya uchaguzi na kfuatiwa kuteuliwa kwa Skauti Mkuu na Mlezi wa Skauti (Rais wa nchi)
 Kipenga cha kumtafuta Skauti Mkuu kimepulizwa, mwisho wa kurudisha fomu ni tarehe 15 Januari, 2018 waweza kujaza fomu kielektronik kwa kubonfya hapa ➤ https://tzcentenary2017.wordpress.com/2018/01/06/fomu-ya-uongozi-chama-cha-skauti-tanzania/ pia waweza kupata fomu ya uongozi kwa barua pepe ya: szone2012@live.com au dsmscout@gmail.com
Waweza pia kupakua fomu hii kwa https://web.facebook.com/SCF360