Ijumaa, 14 Agosti 2015

RAIS PROF. JAKAYA KIKWETE KUUTUBIA SKAUTI

MKUTANO MKUU WA BARAZA KUU TANZANIA

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE MGENI RASIMI


Wakati Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la Chama cha Skauti Tanzania ukianza kwa semina elekezi kwa Viongozi wote wa Skauti Tanzania.

 Viongozi wa Skauti kutoka pande zote za Mikoa ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani waliwasili kuanzia tarehe 12-08-2015 tayari kwa Mkutano Mkuu wa Baraza kuu la Taifa ambapo utakaofanyika siku ya jumamosi, tarehe 15-08-2015 katika Ukumbi wa Karimjee Dar Es Salaam, ambapo Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa Professor Jakaya Mrisho Kikwete atakuwa mgeni rasimi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pia ni Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania Prof. Jakaya Kikwete

Pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwepo pia watakuwepo viongozi wa Chama cha Skauti Tanzania, rais wa Chama cha Skauti Tanzania Dkt. Shukuru Kawamba (waziri wa Elimu na Ufundi), Skauti Mkuu Mheshimiwa Mwantum Mahiza (Mkuu wa Mkoa wa Lindi), Kamishna Mkuu Mheshimiwa Abdulkarim Shah (Mbuge wa Mafia - anayemalizia muda wake), Naibu Kamishna Mkuu Ndugu Rashid Mchatta, Mwenyekiti wa Kamati Tendaji Balozi Nicholaus Kuhanga, pamoja na Ma-kamishna wote wa Mikoa na Wilaya wa Skauti Tanzania.

Katika mkutano huo ambapo Rais J. Kikwete atachukua nafasi ya kuwaaga Skauti Tanzania, wito umetolewa kwa wadau na marafiki wa Skauti kujumuika kwa pamoja katika tukio hilo linalotarajiwa kuanza saa 2 asubuhi ya tarehe 15-08-2015, Jumamosi katika Ukumbi wa Karimjee Dar Es Salaam.

Sambaza Upendo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni