Jumapili, 12 Februari 2017

Matembezi ya Hisani (Scouts Charity Walk 2017)



Chama cha Skauti Tanzania kuelekea kusherehekea Siku ya Skauti Afrika na kuazimisha miaka 100 tangu Skauti kuingia Tanzania Bara (Tanganyika).

Skauti ulianza mwaka 1917 na mwaka huu wa 2017 Skauti inatimiza miaka mia moja, Kwa kutaka kufanikisha zaidi Chama cha Skauti Tanzania kimeandaa matembezi ya hisani (Charity Walk) ili kuweza kupata fedha kutoka kwa wadau na marafiki wa Skauti.

Pamoja na matembezi hayo ya hisani yenye lengo la kukusanya pesa za matukio hayo makubwa ya Kitaifa, Chama cha Skauti Tanzania (TSA) pia imeandaa chakula cha kuchangisha fedha kwa mazumuni hayo hayo katika kusaidia watoto na vijana kufanikisha dhima yao.

Matembizi ya hisani yatafanyika siku ya Jumamosi tarehe 18 mwezi wa Februari 2017 kuanzia katika kiwanja cha Skauti kilichopo Upanga barabara ya Malik na kuishia katika bwalo la Polisi la Oysterbay kuanzia saa 12 asubuhi.

Matembezi hayo ya hisani yataongozwa na Mdhaminiwa Skauti Tanzania Mh. A. H. Mwinyi (Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania).
Mheshimiwa Mwinyi amekuwa akiongoza matembezi mengi ya hisani hapa Tanzania, hii ni kwa kuwa ni mtu ambaye anapenda sana kufanya mazoezi.

Uchangishaji fedha kwa njia ya chakula (Dinner Gala Fundraising) inategemea kufanyika tarehe 24 Februari 2017 katika hioteli ya Serena iliyopo jijini Dar es Salaam.

Matembezi hayo ambayo mtandao mkubwa na mpana wa kijamii wa Skauti Scouts Chat Forum (SCF360) imeyapa jina la kuamasisha la #NiMatembeziYe2 katika kuamasisha katika mitandao ya kijamii na kuwesambaza picha mbalimbali za uamasishaji.



Siku ya Skauti Afrika inatarajiwa kufanyika tarehe 8 hadi 11 Machi, 2017 Arusha katika kitongoji cha Kisongo.

Alikadhalika Miaka 100 ya Skauti Tanzania pia yatafanyika Kisongo, Arusha kuanzia tarehe 24 Jun1 hadi 1 julai 2017 na matukio yote mawili yanatarajiwa kuhudhuriwa na Skauti kutoka ndani na nje ya Tanzania (Afrika na nje ya bara la Afrika)

Kwa Usajili na habari zaidi waweza kutembelea kurasa hizi:-